Hatua zisipochukuliwa, tunaelekea kuwa na vipaza sauti badala ya vyombo vya habari

By Bin mazrouy

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekipiga faini ya TZS milioni 10 kituo cha TV cha ITV

ITV imepigwa faini hiyo kutokana na na kipindi kutoka bungeni kilichokuwa kinaendesha mahojiano ya moja kwa moja ambapo Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Petter Msigwa alisikika akisema “Naibu Spika amekuwa kama anavaa pampas, hataki kubanduka kwenye kiti kuongoza bunge”.

Kauli hii ya Mchungaji Msigwa imetafsiriwa kama ni kauli ya kuudhi, na imesababisha ITV kuangukiwa na rungu zito la faini badala ya mtoaji wa kauli hiyo.

TCRA wanadai katika mahojiano hayo muongozaji wa kipindi alishindwa kusimamia mjadala uliokuwa ukiendelea na kuruhusu mgeni wake kutoa kauli yenye kuudhi.

TCRA hawakuitendea haki ITV katika maamuzi haya, ukizingatia kuwa kipindi kilikuwa kinarushwa moja kwa moja (Live) na mtangazaji hajui Source wake anakwenda kuzungumza kitu gani juu ya kile alichomuuliza, hivyo kukosa nafasi yaq kuhariri kile kinacho onekana kuudhi.

Kinacho onekana katika maamuzi haya ni muendelezo wa vitisho kwa vyombo vya habari dhidi ya kile kinachoonekana kuwa ni kuwakosoa viongozi wenye mamlaka ya uendeshaji wa vyombo vya maamuzi ya wananchi.

Kwa hali hii sasa vombo vya habari vitaacha kuandaa vipindi na mijadala na mijadala yenye kuikosoa serikali na viongozi wake kwa maslahi mapana ya taifa kwa kuhofia rungu la adhabu za faini ama hata kunyimwa kabisa leseni ya kuendeshea vyombo hivyo kutoka kwa wenye mamlaka ya kufanya hivyo.

Ikiwa hali hii itaachwa iendelee tutarajie vyombo vyetu vya habari kuwa vipaza sauti tu vya watawala kufikisha ujumbe wao kwa watu wa chini badala ya kuwa majukwaa yenye kuibua hoja za kujenga taifa letu.

Ili kuepusha vyomba vya habari kuwa vipaza sauti vya watawala ipo haja kwa wadau wa habari kupingana na viashiria hivi vya vitisho vinavyo zidi kutolewa kila siku dhidi ya vyombo vya habari na watendaji wake kwa maslahi mapana ya taifa letu.

 

Masheikh wana wajibu wa kuisaidia jamii katika kukuza elimu

Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi kwa niaba ya Rais wa Zanzibar akiufungua  Msikiti wa Kijiji cha Kajengwa utakaotoa huduma za ibada za sala na madrasa kwa waumini wa Kijiji hicho.
Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi kwa niaba ya Rais wa Zanzibar akiufungua Msikiti wa Kijiji cha Kajengwa utakaotoa huduma za ibada za sala na madrasa kwa waumini wa Kijiji hicho.

Na Othman Khamis Ame – OMPR

Wanazuoni, Masheikh na wazee wote nchini wana wajibu mkubwa wa kuisaidia Serikali Kuu katika jitihada zake za kukuza elimu, kujenga jamii iliyo bora, kulinda amani pamoja na kukataza maovu vikiwemo vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji wa kijinsia.

Kauli hiyo imetolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al – hajj Dr. Ali Mohamed Shein wakati akiufunguwa msikiti wa Kijiji cha Tasani  Makunduchi unaokadiriwa kusaliwa na waumini wapatao 200 kwa wakati mmoja wa sala.

Dr. Shein ambae Hotuba yake ilisomwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema katika msaada huo Masheikh wana fursa nzuri ya kuzungumza na waumini wao hasa kupitia hotuba za sala za ijumaa ili kujenga jamii iliyo bora.

Alisema Dini imekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa zaidi kwenye suala zima la kukuza maadili mema , malezi ya watoto sambamba na kuendeleza hali ya kuishi kwa upendo miongoni mwa jamii  yote.

Rais wa Zanzibar alieleza kwamba Serikali imedhamiria kutilia mkazo mfumo wa Utawala bora unaozingatia utii wa sheria na kuendeleza mikakati katika kuimarisha uwajibikaji kwa kupiga vita ubadhirifu wa mali za umma.

Alifahamisha kwamba uimarishwaji wa mafunzo ya dini katika misikiti na hata madrasa una mchango mkubwa katika kuisaidia Serikali kuimarisha lengo lake hilo la usimamizi wa Utawala bora pamoja na utekelezaji wa mipango ya maendeleo.

Al Hajj Dr. Ali Mohamed Shein amewapongeza Waumini na Wananachi wa Makunduchi kwa jitihada zao walizochukuwa na hatimae kufanikiwa kupata nyumba mpya ya Ibada.

Alisema Jamii imekuwa  ikushuhudia ongezeko kubwa la ujenzi wa misikiti mikubwa yenye nyenzo za kisasa katika pembe zote za Visiwa vya Unguja na Pemba neema ambayo Mwenyezi Muungu anaendelea kuishusha ndani ya Nchi hii.

Alieleza kwamba ujenzi wa Misikiti mipya ni ishara ya kuendelea kwa imani na mapenzi baina ya waislamu pamoja na kuongezeka kwa nguvu za kiuchumi miongoni mwa wananchi.

Dr. Shein aliikumbusha jamii kujitokeza zaidi katika kuwekeza katika mambo ya kheri kama hili la ujenzi wa misikiti ili kujitengenezea maisha bora ya baadaye na kuachana haya ya duniani ambayo ni ya mpito.

“ Na simamisheni sala na mtoe zaka na mkatieni Mwenyezi Muungu sehemu njema { katika mali yeni iwe ndio zaka na sadaka } na kheir yoyote mnayoitanguliza kwa ajili ya nafsi yenumtaikuta kwa mwenyezi mungu imekuwa bora zaidi na ina thawabu kubwa sana “. Dr. Shein aliikariri suratul Muzzammil aya ya 20.

Alisema ni vyema kwa waliojaaliwa uwezo kuangalia maeneo wanayoishi namna bora ya kutoa sadaka inayoendelea katika kupitia usambazaji wa huduma zinazohitajika na jamii iliyowazunguuka.

Alieleza kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikitekeleza dhamira ya kuhakikisha kuwa wananchi wake wanapata huduma muhimu katika maeneo wanayoishi.

Hata hivyo alisema zipo sababu tofauti zinazochangia kwa kiasi kikubwa baadhi ya wananchi kuendelea kukosa huduma hizo muhimu kwa maendeleo yao ya kijamii ya kila siku.

Aliwapongeza waislamu wote waliochangia pamoja na kushiriki kwenye ujenzi wa msikiti huo juhudi ambazo lazima ziambatane na kuendelea kuutunza  msikiti huo ili uendelee kubakia katika haiba yake ya kupendeza.

Katika kuunga mkono juhudi za waumini hao Balozi Seif  Ali Iddi Binafsi aliahidi kusaidia pampu ya kusukumia maji katika msikiti huo mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa mnara wa tangi la maji.

Mapema asubuhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwa Niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi alilifungua jengo la Madrasatul Shafiat liliopo katika Kijiji cha Kajengwa Makunduchi.

Akizungumza na waumini hao Dr. Shein alisema ufunguzi wa madrasa hiyo ni kielelezo cha jitihada za wananchi wa kajengwa kwa kushirikiana na viongozi wao katika kutilia maanani haja ya kuwapatia elimu ya dini watoto wao jambo ambalo limefaradhishwa na mwenyezi mungu.

Alisema elimu nizawadi na urithi bora kwa watoto ambao huwajenga kuwa na ucha mungu, kujua utu, kuheshimu haki za watu wenye  imani za dini nyengine sambamba na kumtukuza mola anayeteremsha neema kwa viumbe wote.

Alitoa wito kwa uongozi wa Madrasatul Shafiat kufanya juhudi za makusudi kuisajili Madrasa hiyo ili ifuate taratibu zilizopo pamoja na kutambulika rasmi kiserikali.

Alisema Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kupitia kitengo kinachosimamia elimu ya maandalizina madrasa huzisajili madrasa ili kuzitambua , kusimaia taaluma inayotolewa , kuzipatia misaada ya kitaaluma vikiwemo pia vifaa.

Katika juhudi za kuunga mkono waumini hao wa Kajengwa Makunduchi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa niaba ya Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohd Shein aliahidi kuchangia mafeni yote ya Madrasat Shafiiya, Meza ya Mwalimu, pamoja na Makabati ya Vitabu vya Madrasa hiyo.

Akisoma risala ya walimu na Wanafunzi hao wa Madrasat Shafiiya Mwalimu Abou Simai Mussa alisema madrasa hiyo yenye wanafunzi karibu 150 inatoa mafunzo ya elimu ya Dini na Dunia.

Mwalimu Abou alisema madrasa hiyo hivi sasa imekuwa chem chem. Kubwa ya utoaji wa walimu na masheikh mbao wamekuwa wakitoa mafunzo ya kuongoza ibada katika misikiti mbali mbali ya Jimbo la Makunduchi.

Alimpongeza Mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi kwa jitihada zake za kuchangia ujenzi wa msikiti huo zilizofikia zaidi ya asilimia 99% ukigharimu zaidi ya shilingi Milioni 21.3.

Akitoa shukrani kwa niaba ya wananchi na waumini hao wa Jimbo la Makunduchi Mwakilishi wa Jimbo Hilo Al Hajj Haroun Ali Suleiman alisema Uongozi wa Jimbo hilo utaendelea kushirikiana na wananchi hao katika kuhakikisha kwamba kero zinazowakabili zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Al – Haroun alisema tatizo la huduma za maji safi na salama ambalo limekuwa kero kubwa kwa wananchi hao hasa katika eneo la ibada la Msikiti atalishughulikia kwa kushirikiana na viongozi wenzake wa jimbo hilo.

Mapema Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Ngwali aliwakumbusha waumini hao kwamba Madrasa lazima zitumiwe kwa juhudi zote katika kujenga hatma njema  ya dunia na sfari ya milele.

DUNI: Mahujaji hawakuipigia kura katiba inayopendekezwa

Wanachama wa Chama cha Wananchi CUF wakimsikiliza Makamo Mwenyekiti wa Chama hicho , Mh, Juma Duni Haji (hayupo pichani) katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Amani kwa mabata.
Wanachama wa Chama cha Wananchi CUF wakimsikiliza Makamo Mwenyekiti wa Chama hicho , Mh, Juma Duni Haji (hayupo pichani) katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Amani kwa mabata.

Na Nassor Khamis.
Suala la wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba waliokuwa kwenye ibada ya Hijja katika miji ya Makka na Madina chini Saudi Arabia, kupigia kura rasimu ya katiba inayopendekezwa na Bunge hilo sikweli.

Hayo yalielezwa na Makamo mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF taifa Mh, Juma Duni Haji wakati akizungumza na wanachama wa chama hicho katika viwanja vya Amani kwa mabata wilaya ya Magharibi Unguja.

Mh, Duni ambaye pia ni Waziri wa Miundo mbinu na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar alisema, kulingana na hali ilivyokuwa katika ibada ya hijja ni vigumu kwa wajumbe hao kupiga kura kwa njia yoyote kutokana na muda wote kuwa katika ibada.

“Suala la kupigwa kura kwa njia ya mtandao ni uongo kwani hakuna hata mtu mmoja aliyepiga kura kutokana na muda wote kuwa katika ibada” alisema Mh, Duni

“Mimi nilikuweko wakati tupo katika mabanda yetu mahujaji nilimuuliza mmoja wa wajumbe vipi ndio utapigia kura katiba hapa” aliongezaMh. Duni.

Pia alisema kuwa licha ya mahujaji hao kushindwa kupiga kura kwa njia ya mtandao, hakuna afisa yoyote aliyeweza kuendesha zoezi la upigaji kura kutokana na kutokuruhusiwa kuingia kwa mtu yoyote asiyekuwa mwenye kufanya ibada hiyo ya hijja.

Aidha amesema kuwa kutoka na mahujaji hao kutokupiga kura na wengine waliyoikata hadharani theluthi mbili ya wazanzibari ya kupitisha katiba inayo pendekezwa haikutimia.

Akizungumzia Katiba inayopendekezwa alisema, katiba hiyo haina maslahi kwa Zanzibar kwani Katiba inayopendekezwa inafuta utambulisho wa Zanzibar pamoja na kuinyima Zanzibar mamlaka yake ya kujiendesha wenyewe.

Alisema kuwa baadhi ya vipengele vinavyoonyesha kuipa mamlaka Zanzibar ni sawa na kupewa kitu kwa mlango wa mbele na kisha kunyang’anywa kwa mlango wa nyuma kwani vipengele hivyo vipo chini ya mamlaka ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Vipengele hivyo amevitaja kuwa ni pamoja na Zanzibar kujenga mashirikiano na mashirika ya kimataifa pamoja na uwezo wa kukopa fedha kutoka taasisi mbali mbali za kifedha hadi ipate udhamini kutoka kwa Serikali ya Muungano.

“Eti wanasema sasa Zanzibar inaweza kukopa pamoja na kujiunga na mashirika ya kimataifa baada yakupata udhamini ikiwa huo udhamini haukutolewa pamepatikana kitu hapo?” alihoji Mh, Duni.

Pia alisema kuwa kutokana katiba mpya inayopendekezwa kubainisha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atachaguliwa kwa kupata zaidi ya asilimia hamsini ya kura zote ni vigumu kwa Mzanzibari yoyote kushika wadhifa huo kutokana na idadi kubwa ya wapiga kura walioko Tanzania Bara.

Alisema kuwa ili kupata uhalali wa Rais wa Muungano, Katiba inayopendekezwa iweke kifungu kinacho onesha kiwango maalum cha kura kutoka kwa wapiga kura wa pande zote za Muungano.

Mh. Duni pia alizungumzia vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji unaofanywa na jeshi la polisi kwa watuhumiwa makosa ya ugaidi huku viongozi wa serikali wakikaa kimya, ni kushindwa kusimamia haki za wananchi wanaowaongoza.

Akitolea mfano wa vitendo vya udhalilishaji kwa watuhumiwa wa makosa mbalimbali yaliyowahi kufanyika huko nyuma askari waliofanya vitendo hivyo walichukuliwa hatua za kisheria ikiwamo kufukuzwa kazi.

Amesema kuwa wakati wa uongozi wa awamu ya kwanza wa Jamhuri Muungano wa Tanzani vitendo vya udhalilishaji wa watuhumiwa waliokuwa mahabusu jijini Mwanza Mwalimu Nyerere aliwawajibisha maafisa wa jeshi la polisi kwa kuwafukuza kazi huku aliyekuwa Waziri wa Mambo ya ndani wakati huo Mzee Ali Hassan Mwinyi kulazimika kujiuzulu wadhifa wake.

“leo wanakuja raia mahakamani wanaonesha suruali zinavyovuja chini kutokana na vitendo vya udhalilishaji wanavyofanyiwa na Polisi wewe husemi kitu Rais gani wewe” alisema Mh. Duni.

Aidha mh, Duni ametaka sheria zilizotungwa zifuatwe kama inavyostahiki pamoja na kuheshimiwa na watu wote.

Akizungumza katika mkutano huo Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar Mh, Nassor Ahmed Mazruy alisema kifungu cha thalathini na nne cha sheria ya mabadiliko ya katiba inayosema kuwa katiba inayopendekezwa itapitishwa kwa zaidi ya asilimia hamsini ya kila upande kimelenga kuchakachua kura za maoni ya kupitishwa kwa katiba hiyo.

Alisema kuwa kifungu hicho pia kinawataka Wazanzibari walioko Tanzania Bara kupiga kura upande wa Zanzibar jambo ambalo haliingia akilini na ina lengo la kuvuruga idadi ya wazanzibari ili waweze kupitisha katiba hiyo.

Aidha alisema kuwa chama cha CUF pamoja na vyama vyengine vya upinzani vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA kwa pamoja wamesaini mkataba wenye lengp la kushirikaiana katika chaguzi mbalimbali ukiwemo uchaguzi wa serikali za mitaa pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kwa lengo la kuindoa CCM madarakani.

Mapema Mjumbe wa Baraza kuu la Uongozi la CUF Taifa ambae pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Ole Mh, Hamad Massoud Hamad amewataka wanachama wa chama hicho kujiweka tayari kwa uchaguzi mkuu ujao kwa lengo la kuiondoa CCM madarakani.

Amesema kuwa uchaguzi unaofuata chama cha CUF hakitofanya makosa kama chaguzi zilizopita kwa kukubali matokeo yasiyo halali yanayo tangazwa na tume ya uchaguzi Zanzibar kwa kutoa ushindi usiostahiki kwa CCM.

“Uchaguzi wa safari hii CUF haifanyi makosa kama yaliyopita viongozi wa juu tayari wameshajiandaa na nyinyi wananchi jiandaeni tuhakikishe tunaing’oa madarakani CCM ifikapo mwakani” alisema Mh, Hamad huku akishangiriwa na wanachama waliohudhuria mkutano huo.

Wazanzibari watakiwa kuipigia kura yandio Katiba inayopendekezwa

Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wakimsikiliza Makamo Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar Dkt, Ali Mohammed Shein (hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara Kibanda maiti mjini Unguja.
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wakimsikiliza Makamo Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar Dkt, Ali Mohammed Shein (hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara Kibanda maiti mjini Unguja.

Na Nassor Khamis, Zanzibar.
Wananchi wa Zanzibar wametakiwa kuipigia kura ya ndio Katiba inayopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba kwani imezingatia maslahi ya Zanzibar ikiwamo masuala ya kiuchumi na kijamii.
Hayo yameelezwa na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein wakati akihutubia kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho katika viwanja vya demokrasia Kibanda maiti mjini Unguja.
Dkt. Shein ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mnzi Mapinduzi amesema katiba inayopendekezwa imetatua kero zote za Muungano zilizokuwepo na kuzitafutia ufumbuzi ikiwamo kero ya muda mrefu kuhusu suala la mafuta na gesi.
Amesema kuwa suala la mafuta na gesi limekuwa likizungumzwa kwa muda mrefu ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutaka litolewe katika orodha ya mambo ya Muungano ili Zanzibar iweze kukua kiuchumi.
“Suala hili la mafuta na gesi limekuwa likizungumzwa kipindi kirefu na serikali ya Zanzibar tokea nikiwa Makamo wa Rais kule bara na likakubaliwa litolewe na mimi nilipokukuja nimekuta limekubaliwa na mimi nikakubali” alisema Dkt. Shein.
Amesema kuwa kupitia katiba inayopendekezwa suala la hilo tayari limesahatolewa na kuwa chini ya mamlaka ya serikali ya mapinduzi Zanzibar ili kuiwezesha Zanzibar kupiga hatua kiuchumi.
Amesema kuwa makampuni kadhaa ya mafuta yakiwemo kutoka Uholanzi na Ras Al-khaimah yameonesha nia ya kufanya utafiti wa mafuta katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar na hatimae kuyachimaba na tayari makubaliano ya awali ya kazi hiyo yamefikiwa.
Mbali na suala hilo Dkt Shein amezungumzia maswala ya ushirikiano wa Zanzibar na taasisi pamoja na Mashirika ya kimataifa kuachwa katika mamlaka ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar jambo litakalo saidia katika maendeleo ya nchi na wananchi wake.
Aidha amesema kuwa, kupitia katiba inayopendekezwa Zanzibar imeruhusiwa kukopa fedha katika mashirika na taasisi mbalimbali ikiwemo kupata udhamini wa Serikali ya Muungano pale itakapohitajika na itapatiwa udhamini huo.
Akizungumzia mchakato wa katiba mpya Dkt. Shein amesema mchakato huu umeendeshwa kawa mashirikiano makubwa kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tokea uundwaji wa sheria ya mabadiliko ya katiba hadi hatua iliyofikia.
Pia amewataka wananchi kuendeleza amani iliyopo na wasikubali kugawiwa kwa misingi ya katiba mpya kwani katiba inayoandikwa imetokana na makubaliano ya pande zote.
Pia amesisitiza kuwa serikali haitafumbia macho vitendo vyovyote vinavyo ashiria uvunjifu wa amani na itailinda amani ya nchi kwa gharama yoyote.
Nae Waziri wa fedha na uchumi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh, Saada Salum Mkuya amesema katiba inayopendekezwa imezingatia maslahi ya Zanzibar katika masuala yote yakifedha ikiwemo mapato ya serikali yatokanayo na kodi ya mambo ya Muungano.
Amesema kuwa mapato yote yanayokusanywa kama kodi ya mfanya kazi wa taasisi za Muungano zilizopo Zanzibar yatabakia katika serikali ya Zanzibar kwa maendeleo ya Zanzibar.
Akizungumza katika mkutano huo aliyekuwa Makamo Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh, Samia Suluhu Hassan amesema katiba inayopendekezwa imetoa fursa sawa za kiuongozi kati ya Tanzania bara na Zanzibar hasa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani endapo Spika wa Bunge hilo akitoka bara Naibu wake atatokea Zanzibar.
Mh, Samia ambae pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais anaeshughulikia Muungano amesema, inayopendekezwa imetoa fursa kwa wanawake kwa kutoa haki sawa katika nafasi zote za uongozi wa nchi kwa asilimia hamsini kwa hamsini baina ya wanawake na wanaume pamoja haki ya uzazi salama kwa kina mama.
Mapema akizungumza katiaka mkutano huo Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Hamid Ameir amemtaka Mzee Hassan Nassor Moyo aache kuwapotosha Wazanzibar kuhusu Mapinduzi ya 1964 kutokana nakuwa hakuwa mshiriki wa Mapinduzi hayo.
Mapema katika Risala yao wanachama wa CCM wa mikoa minne ya kichama ya Unguja wameunga mkono mapendekezo yaliyomo katika Katiba inayopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba lililomalizika mwanzoni mwa mwezi huu mjini Dodoma.
Mkutano wa CCM umekuja baada ya mikutano miwili tofauti iliyofanywa na Chama cha Wananchi CUF hivi karibuni katika viwanja vya Demokrasia Kibanda maiti mjini Unguja na viwanja vya Gombani ya kale kisiwani Pemba.
Mikutano yote hiyo ilihutubiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho ambae pia ni Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad na viongozi kadhaa wa Chama hicho.

Maalim Seif: Katiba inayopendekezwa inainyima mamlaka Zanzibar

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Demokrasia Kibanda Maiti Zanzibar.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Demokrasia Kibanda Maiti Zanzibar.

Na Nassor Khamis.

Wananchi wa Zanzibar wametakiwa kupiga kura ya hapana kwa Rasimu ya katiba inayopendekezwa kutokana na kutozingatia maslahi ya Zanzibar.

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Demokrasia Kibanda maiti mjini Unguja.

Akivizungumzia baadhi ya vifungu Maalim Seif amesema katiba inayo pendekezwa imepunguza mamlaka zaidi ya Zanzibar tofauti na ilivyoelezwa na wanaounga mkono katiba hiyo.

Amesema kuwa katiba inayopendekezwa imetoa mamlaka zaidi kwa Serikali ya Muungano kwa kusema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi moja yenye mamlaka kamili hivyo kuinyang’anya Zanzibar mamlaka iliyo nayo kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar toleo la 2010.

Maalim Seif amesema kuwa Katiba ya Zanzibar inampa uwezo Rais wa Zanzibar kuigawa Zanzibar katika Mikoa na maeneo mengine ya kiutawala ambapo kwa sasa mamlaka hayo yamewekwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha amesema kuwa rasimu hiyo bado haijatoa uhuru kwa Zanzibar kushirikiana na Mashirika na Jumuiya za kikanda pamoja na Kimataifa kutokana na mashirika hayo kutoa uwanachama kwa nchi zenye mamlaka kamili ya kiuongozi jambo ambalo kwa Zanzibar bado halijapatikana.

“Shirika kama la Chakula duniani, UNESCO na mashirika mengine hatoi uanachama kwa nchi ambazo hazina mamlaka ya kujiendesha wenyewe na kwa Katiba hii inaqyopendekezwa bado Zanzibar haijapata mamlaka kamili” alisema Maalim Seif.

Aidha amesema kuwa Rasimu iliyotolewa na Tume ya jaji Warioba ilipunguza idadi ya mambo ya Muungano kutoka 22 hadi kufikia saba badala yake Rasimu inayopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba imeyaongeza kutoka saba hadi 14.

Pia amesema kuwa Rasimu inayopendekezwa bado imeifanya Ta nganyika kuendelea kuvaa koti la Muungano kutokna na mambo yake yasiyokuwa ya Muungano kuendelea kusimamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pia amesema kuwa katiba inayo pendekezwa imekosa uhalali wa kisheria kutokana na kutopatikana kwa theluthi mbili ya wajumbe kutoka Zanzibar waliyoinga mkono rasimu hiyo wakati wa upigaji wa kura.

Amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Katibu wa Bunge Maalum la Katiba Yahya Khamis Hamad wajumbe waliopiga kura ya ndio hawakufikia theluthi mbili badala yake matokeo yaliyotangazwa yalikuwa na lengo la kuipitisha rasimu hiyo kinguvu kwa maslahi ya Chama cha Mapinduzi.

Aidha amesema kuwa endapo katiba inayopendekezwa itapitshwa itasababisha mgogoro wa kikatiba kutokana na na katiba hiyo kukinzana na katiba ya Zanzbar hivyo kulazimisha kufanyiwa marekebisho katiba ya Zanzibar jambo ambalo halitawezekana.

Amesema kuwa ili kuifanyia marekebisho katiba ya Zanzibar kutahitajika theluthi mbili ya Wajuumbe wa Baraza la Wawakilishi kuunga mkono ambapo wajumbe watokanao na chama cha CUF hawatakubali jambo hilo kutokea.

Akizungumza katika mkutano huo Naibu Katibu Mkuu wa CUF Mh, Nassor Ahmed Mazrouy amewataka Wazanzibar kuikataa katiba inayo pendekezwa pamoja na kuwakataa Wabunge na Wawakilishi wote waliopiga kura ya ndio kwa katiba inayo pendekezwa.

Naye Mjumbe wa kamati ya maridhiano Mansour Yussuf Himid amesema kuwa ataendelea kuitetea Zanzibar ipate mamlaka yake kamili hivyo ataendelea kupingana na mfumo wa Muungano wa CCM uliojaa ukatili dhidi ya Wanzibari.

Alisema kuwa kwa mujibu wa vitabu vya dini mbali mbali vinaeleza kila nafsi itaonja mauti je wao wanaogopa nini kilichobakia ni kuingia mitaani kuwambia Wazanzibar wasikubali kuipitisha katiba hiyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Maridhiano Zanzibar,Mzee Nassor moyo alisema kuwa Wazanzibar waliungana na Tanganyika kwa hiari yao hivyo hakuna mtu yeyote wa kuwalazimisha kufanya mambo yanayokwenda kinyume na matakwa ya Wazanzibar.

Mapema mkurugenzi wa habari na uenezi wa CUF, Salim Abdallah Bimani alisema kuwa rasimu inayopendekezwa sio ya wazanzibar na haitofika Zanzibar bali itaishia Kisiwa cha Chumbe .

Na aliwataka wazanzibari kuungana pamoja na kuikataa kwa nguvu zote rasimu ya Chenge na wenzake kwani imekuja kuangamiza Zanzibar.

Kura ya hapana yatikisa Bunge Maalumu la Katiba

Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta,  akiwaonyesha wajumbe wa bunge hilo, karatasi za kupigia kura zitakazotumika kupitishia vifungu vya Rasimu ya Katiba,  bungeni,Dodoma jana.
Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta, akiwaonyesha wajumbe wa bunge hilo, karatasi za kupigia kura zitakazotumika kupitishia vifungu vya Rasimu ya Katiba, bungeni,Dodoma jana.

Wajumbe wa Bunge la Maalumu la Katiba jana walianza kupiga kura za kuamua ibara za Katiba inayopendekezwa, huku kura za wajumbe kutoka Zanzibar zikiibua wasiwasi wa iwapo theluthi mbili itapatikana au la.

Dalili za kupiga kura za hapana kutoka upande wa Zanzibar zilianza kujionyesha mapema baada ya taarifa za ndani kueleza kuwa zikikosekana 10 kutoka upande huo wa Muungano hakuna katiba.

Hata hivyo, mapema Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta alisema idadi ya kura zinazohitajika kukidhi theluthi mbili kwa upande wa Zanzibar ni 140 na jana jioni waliokuwamo bungeni walikuwa 142.

Mjumbe wa kwanza kufungua pazia kwa kura ya hapana alikuwa ni Adil Mohamed Adil aliyepiga ibara zote 157 kwa sura ya kwanza hadi 10.

Wengine waliopiga kura ya hapana kwa sura zote ni Dk Alley Soud Nasoro na Salma Said.

Waliopiga kura za hapana ni Fatuma Mohamed Hassan na Jamila Abeid Saleh, huku baadhi ya wajumbe wakipiga kura za siri.

Kwa upande wake, Ali Omary Juma, alikubaliana na sura za 2, 4, 5 na 9 lakini akizikataa sura za 1,3,6,7,8 na 10.

Kwa upande wa Tanzania Bara, wajumbe Abia Nyabakari na Dk Ave-Maria Semakafu walipiga kura za ndiyo kwa baadhi ya sura na zingine kuzikataa.

Mjumbe Ali Keissy Mohamed aliushangaza ukumbi kwa kupiga kura ya ndiyo kwa sura zote tofauti na wakati akiwa katika vikao vya kamati ambapo alikataa muundo wa serikali mbili.

Watakaopiga kura kwa faksi

Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta jana alitangaza orodha ya wajumbe 22 wanaotarajiwa kupiga kura kwa njia ya faksi au mtandao wakiwa nje ya Bunge hilo.

Katika orodha hiyo, akiwamo Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Fredrick Werema, wajumbe tisa wako Saudi Arabia kwa ajili ya Hijja, wawili India kwa matibabu, mmoja yuko masomoni Uholanzi na wengine nje ya Dodoma lakini yuko hapa nchini.

Orodha ya wajumbe

Wajumbe walioko Uarabuni ni Dk Abdalah Kigoda, Mussa Yusuph Kundecha, Hamza Mustapha Njozi, Mohamed Raza, Dk Maua Daftari, Shawana Bukheri Salum, Asha Dodo Mtwangi, Amina Andrew Clement na Riziki Lulida.

Wajumbe walioko India kwa matibabu ni Beatrice Shelukindo na Salum Hassan Turk.

Wajumbe wengine waliko nje ya nchi ni Fredrick Msigala, Waziri wa Afya, Dk Seif Suleiman Rashid, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela na Waziri Mkuu Mstaafu, John Malecela.

Waliopo nchini ni Esther Bulaya, William Lukuvi, Profesa Esther Mwaikambo, Dk Athman Mfutakamba, Saada Salum Mkuya, Dk Henry Nyamubi, Sixtus Mapunda na Dk Natujwa Mvungi.

Mwananchi.

Mahakama ya Kadhi yalitafuna Bunge

Wabunge wakiwa Bungeni mjini Dodoma
Wabunge wakiwa Bungeni mjini Dodoma

Suala la Mahakama ya Kadhi limechafua hali ya hewa bungeni mjini Dodoma baada ya wajumbe Waislamu kutishia kupiga kura ya hapana kama halitaingizwa katika Rasimu inayopendekezwa.

Wakati Waislamu wakishikilia msimamo huo, wajumbe ambao ni Wakristo nao wamejipanga kupiga kura ya hapana endapo Mahakama ya Kadhi itaingizwa katika Katiba inayopendekezwa.

Dalili za mpasuko huo zilianza kujitokeza jana asubuhi baada ya mjumbe mmoja, Jaku Ayub Hashim kuwasha kipaza sauti akitaka kuzungumza akisema ana jambo muhimu.

“Mheshimiwa tangu jana (juzi) ulisema utanipa nafasi ya mwanzo nizungumze,” alisema Jaku, lakini Makamu Mwenyekiti, Samia Suluhu alimtaka aketi chini na suala lake limesikika.

Suluhu akaendelea kuwapa wajumbe wengine kuendelea kuchangia na baadaye alimpa Jaku muda wa dakika saba ili kuwasilisha kile alichotaka kukizungumza ndani ya Bunge hilo.

Jaku alisema walipendekeza kifungu kinachotaka uamuzi unaohusu ndoa, talaka na mirathi iliyoamuliwa kwa misingi ya dini ingizwe kwenye Katiba inayopendekeza lakini hakimo.

“Ni kitu kidogo kabisa tuliomba kiongezwe lakini cha kusikitisha kikundi cha sanaa kimeingizwa. Mimi binafsi yangu sitaunga mkono wala mguu wala sitaipigia kura hii,” alisema Jaku.

Suluhu akamweleza kuwa angalizo lake limechukuliwa, na uongozi wa Bunge pamoja na kamati ya Uandishi wanajitahidi kuingiza kila kitu kinachowezekana, lakini kwa misingi na sheria za nchi.

Baadaye Sheikh Masoud Jongo alipopewa nafasi ya kuchangia, naye alitahadharisha kuwa mambo yaliyopendekezwa na Waislamu yasipoingizwa kama ilivyo kwa sasa, hawatakuwa tayari kwa lolote.

“Msimamo wetu sisi Waislamu kama mambo yetu tuliyoleta katika mapendekezo hayataingizwa, basi yatabomokea hapa na hatutakuwa tayari tena,” alisema Sheikh Jongo, kauli iliyowashtua wajumbe.

Akihitimisha majadiliano hayo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge alisema kamati yake imefanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kwa masilahi ya Watanzania. Akiahirisha Bunge, Suluhu alisema kesho Bunge litaanza kwa kupitia baadhi ya mambo yaliyoibuka katika uhakiki kisha kupitisha azimio la upigaji wa kura. Kura zitapigwa kati ya kesho hadi Oktoba 2.

Baada ya kuahirishwa kwa Bunge, Sheikh mwingine, Hamid Jongo alimwendea Askofu mstaafu Donald Mtetemela na kumkumbatia, kisha kumvuta pembeni na kisha kuteta kwa dakika tano.

Katika viwanja vya Bunge, hali ilikuwa tete kwani kulikuwa na makundi tofauti tofauti ya Wakristo na Waislamu kila moja likijadili na kutafakari suala la Mahakama ya Kadhi kuingizwa kwenye Katiba.

Mjumbe wa kundi la 201 Dk Aley Nassoro alisema kuwa suala la Mahakama ya Kadhi lisipoingizwa katika Katiba inayopendekezwa, atakuwa wa kwanza kuhamasisha wenzake ili wagome kupiga kura.

Dk Nassoro alisema Waislamu wamechoka kudanganywa kwani tangu kipindi cha kampeni za mwaka 2010, waliahidiwa kuwa jambo hilo lingeshughulikiwa mapema lakini watawala wamekuwa kimya.

“Hii Katiba itakuwa ni mbovu kuliko ile ya mwaka 1977 na italeta migongano baada ya miezi sita tu tangu kuzinduliwa. Bora iachwe kwani mambo mengi ya msingi kwa Wazanzibari yameachwa,”alisema.

Akiwa viwanja vya Bunge Askofu Mtetemela alionekana akishauriana na wajumbe mbalimbali na baadaye alisema analaani kauli hizo na kusema kuwa hazilengi kujenga nchi badala yake zinabomoa.

“Kinachotakiwa ni amani, sasa tukianza kutishiana mambo hayatakwenda maana na sisi Wakristo tutataka mambo yetu yaingizwe humo, tunachohitaji ni amani na si vinginevyo,” alisema Mtetemela.

Askofu Mtetemela alisema kikubwa kinachotakiwa kwa wajumbe ni maridhiano na isiwe vitisho kwa kuwa walianza pamoja hivyo wanapaswa kumaliza pamoja.

Aliitaka Kamati ya Uandishi kutoingiza kabisa jambo hilo katika Katiba na akasema hali ikifikia hapo itasababisha mgogoro wa kimasilahi kwa kila mtu kudai haki yake ndani ya Katiba.

Hata hivyo, aliitaka Serikali kutunga sheria za kutambua uamuzi wa Waislamu wa ndoa, mirathi na umiliki wa rasilimali kwa Waislamu ili yakubaliwe kwenye sheria siyo kwenye Katiba.

Mjumbe mwingine wa Bunge hilo, John Cheyo, alitaka Watanzania kuendelea kuheshimu Katiba ambayo imeweka wazi kuwa Serikali haina dini bali wananchi wake ndiyo wenye dini.

“Kwa sababu ukienda njia hiyo hakuna atakayeshinda. Na sisi Wakristo tuseme bila ‘Canon Law’ (Sheria za Kanisa) hakuna hatupigi kura, tutafika wapi? Ndiyo maana tuliyatenganisha haya mambo,”alisema.

Wakati makundi hayo yakiwa na msimamo tofauti, jana katika viwanja hivyo vya Bunge walisikika Waislamu wakihamasishana kwamba kama ikifika kesho hakuna Mahakama ya Kadhi wasusie Bunge.

Suala la Mahakama ya Kadhi, linaonekana kuwapasua kichwa wajumbe wa Kamati ya Uongozi ambayo juzi na jana zilikutana kutafuta njia ya kulinusuru Bunge hilo na mpasuko huo mkubwa.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho, zilieleza kuwa baadhi ya wajumbe walipendekeza kuitishwa kwa Kamati ya Maridhiano ili kutafuta njia bora itakayonusuru Katiba Mpya kukwama kesho.

Mwananchi.

Warioba: Nitaendelea kuitetea Rasimu, sitakimbilia Ukawa

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba.
Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Katiba Jaji Joseph Sinde Warioba.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema uamuzi wake wa kuitetea Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na tume aliyoiongoza, pamoja na kauli yake ya juzi ya; ‘Tutakutana mtaani’, havimaanishi kwamba atakihama Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Jaji Warioba amesema jana kwamba baada ya kutoa kauli hiyo katika maadhimisho ya miaka 19 ya Kituo cha Sheria na Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), baadhi ya watu wakiwamo makada wa CCM wanaodhani kuwa atajiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika maandamano ya kudai Katiba Mpya iliyotokana na maoni ya wananchi.

Katika kongamano hilo, Jaji Warioba alisema Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba Septemba 24 mwaka huu bungeni mjini Dodoma, imeondoa mambo manne muhimu na mengine mengi yaliyokuwa kiini cha kupata Katiba ya mageuzi.

Akizungumza na gazeti hili Jaji Warioba alisema: “Juzi (jana) niliposema kuwa tutakutana mtaani, nilikuwa namaanisha kwamba tutakutana na Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba katika midahalo, makongamano, semina na katika vyombo vya habari. Sisi tutaendelea kuitetea rasimu tuliyoitoa Desemba mwaka jana. Wao (wajumbe wa Bunge la Katiba), tutakutana nao huko huko ili wawaeleze wananchi sababu za kuondoa maoni yao.”

Jaji Warioba aliyeiongoza Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa miezi 20 ikiratibu na kukusanya maoni ya wananchi na mabaraza ya katiba ngazi mbalimbali, alisema kuwa kamwe hawezi kujiunga na Ukawa unaoundwa na vyama vya Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF, NLD na DP kwa sababu vyama vya siasa viliuteka mchakato huo na kuuharibu.

“Ieleweke kuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba inasimamia katika maoni ya wananchi na haiwezi kuyumba katika hilo. Tutaendelea kusisitiza kuheshimiwa kwa maoni hayo na wale waliyoyabadilisha, lazima wawaeleze wananchi sababu za kufanya hivyo,” alisema.

Aliongeza: “Inashangaza kuona watu wakihusisha kauli yangu ya juzi na kujiunga na Ukawa au vyama vya siasa. Tusubiri tu, ikifika wakati wa kupiga kura ya maoni ili tuone wananchi watakubali rasimu ipi.”

Katika ufafanuzi wake, Jaji Warioba alisema kuwa hata suala la mgombea huru limewekwa masharti mengi yanayoweza kuwa kikwazo kwa mgombea.

“Mgombea huru kawekewa masharti ambayo binafsi naona kama ni ya kumkataa kistaarabu. Suala la muungano nalo pia ni tatizo na bado halijapatiwa ufumbuzi,” alisema.

Mwananchi.

ZLS: Katiba ya wananchi imeporwa na watawala

Rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS) Awadh Ali Said
Rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS) Awadh Ali Said

Rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS), Awadh Ali Said amesema Rasimu ya Katiba inayopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba imepora mamlaka ya wananchi kutokana na kitendo cha kubadilisha vifungu muhimu ikiwamo mfumo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Akizungumza jana na gazeti hili mjini Zanzibar, Awadh alisema kitendo cha kubadilisha mfumo wa Muungano wa serikali tatu kama ilivyokuwa imependekezwa na rasimu ya awali ya Jaji Joseph Warioba ni kuvunja msingi wa nyumbani na kinakwenda kinyume na maoni ya wananchi.

Alisema kwamba mfumo wa Muungano wa Serikali mbili na marekebisho yake yaliyofanyika umekuwepo katika miaka ya nyuma na katika kipindi cha miaka 50, lakini umeshindwa kuondoa kero za Muungano.

“Bahati mbaya mchakato wa katiba umeporwa kutoka kwa wananchi na kumilikiwa na watawala kinyume na matakwa ya wananchi, hatuwezi kupata katiba bora kwa kuweka masilahi binafsi ya vyama.” alisema Awadh.

Awadh ambaye alikuwa Kamishna wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba alisema kitendo cha kubadilisha vifungu vilivyokuwa vimependekezwa katika Katiba ya awali ni sawa na kuondoa maoni ya wananchi kwa vile rasimu ya Warioba ilitokana na maoni ya wananchi wa pande mbili za Muungano kabla kuwasilishwa bungeni Febuari mwaka huu.

Aidha, alisema kwamba wabunge wa Bunge la Katiba kupitia vyama vya siasa wamezingatia masilahi yao binafsi badala ya masilahi ya Taifa na wananchi wake, ndiyo maana wamefuta vifungu muhimu kama kuwapo kwa ukomo wa kugombea ubunge, kiwango maalumu cha taaluma, wananchi kuwa na mamlaka ya kikatiba ya kumwondoa mbunge asiyewajibika kwa madhumuni ya kuimarisha uwajibikaji na misingi ya utawala bora nchini.

“Jambo la msingi Bunge la Katiba livunjwe, liundwe bunge jipya lisiloshirikisha wabunge wanaotokana na vyama vya siasa ili tupate katiba bora na yenye manufaa kwa wananchi wa pande mbili za Muungano wetu,” alisema Awadh.

Akifafanua, alisema hatua ya wabunge kuingiza mambo ya bahari na ardhi katika orodha ya mambo ya Muungano kutaibua kero nyingine mpya, kwa sababu haiwezekani kuondoa mambo ya mafuta na gesi katika orodha ya mambo ya Muungano wakati rasilimali hizo zinapatikana chini ya ardhi katika mwambao wa bahari.

Hata hivyo, upande wake Mwanasheria Mkuu wa zamani, Hamid Mbwezeleni alisema kwamba rasimu ya mwisho ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano siyo mbaya baada ya kufanyiwa marekebisho mbalimbali na kutaka wabunge wa Bunge la Katiba kupewa nafasi ya kukamilisha majukumu yao.

Alisema kwamba, iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakati ikitekeleza majukumu yake hakuna mhimili ambao uliingilia majukumu yake na kushangazwa na kitendo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo kugeuka msemaji mkuu wa Watanzania.

Mwananchi.

Majambazi wapora milioni 30.6 wajeruhi Polisi, Mfanyabiashara

Sajenti Hija Hassan Hija akipatiwa huduma ya kwanza katika Hospitali ya Mnazi Mmoja mara baada ya kujeruhiwa kwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni mjambazi maeneo ya Mlandege.
Sajenti Hija Hassan Hija akipatiwa huduma ya kwanza katika Hospitali ya Mnazi Mmoja mara baada ya kujeruhiwa kwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni mjambazi maeneo ya Mlandege.

Na Tatu Makame, Laylat Khalfan

WATU wawili akiwamo askari mmoja wamenusurika kifo baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi, waliofanikiwa kupora mfuko wa fedha unaosadikiwa kuwa na zaidi ya shilingi milioni 30.
Tukio hilo, lilitokea jana mchana majira ya 8:30 katika Mtaaa wa Mlandege Mkoa wa Mjini Magharibi, ambapo majambazi hao walimvamia mmoja wa wafanya biashara wa Mchele hapa nchini aliyetambulika kwa jina la Salum Issa Suleiman (50), Mkaazi wa Baghani Mjini Unguja ,, ambaye walimpora mfuko wake wa fedha hizo wakati akiwa njiani kuzipeleka benki.
Mfanyabiashara wakati akiwa njiani alijikuta akizingirwa na mojaya gari ndogo na kuanzakushambuliwa kwa risasi ambazo zilimjeruhi sehemu zake za miguuni na ghafla kuanguka na ndipo majambazi hao walipowezakufanikiwa kumpora fedha hizo.
Wakati tukio hilo likitokea mmoja wa askari  polisi wa Kituo cha Malindi Sajenti Hija Hassan Hija, alijaribu kupambana namabambazi hao, lakini alishindwa kufanikiwa baada na yeye kujeruhiwa sehemu ya mkononi na mguuni kutokana kushambuliwa kwa risasi.

Wakizungumza na gazeti hili, waathirika wa tukio hilo,  Mfanya biashara Salum alisema, wakati alipokuwa akielekea maeneo ya Benki hiyo  ndipo ilipotokea gari ndogo mbele yake na kumnadia mwizi na hapo ndipo walipompiga risasi ya mguu wa kulia na kumnyang’anya fedha hizo na kuondoka nazo .
Kwa upande wake askari Hija alisema, alipofika maeneo hayo ndipo alipomkuta Mfanyabiashara huyo akiwa katika harakati za kujinasua na  hali  na ndipo askari huyo alipokwenda kumuokoa lakini na yeye alishambuliwa na majambazi hao na kufanikiwa kuondoka na kitita hicho cha fedha zamfanyabiashara huyo,,
Hata hivyo,  majeruhi hao bado wanaendelea kupata matibabu katika Hospitali kuu ya Mnazi mmoja na hali zao walieleza kuwa zinaendelea vizuri.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi,  Mkadam Khamis Mkadam, alisema ni kweli tukio hilo limetokea  na aliyeporwa fedha hizo ni  Mfanyabiashara   wa Mchele katika maeneo ya Bandarini ambae alikuwa akielekea katika Benki ya PBZ tawi la Mlandege.
Alisema mfanyabiashara huyo alikuwa na fedha zenye thamani ya shilling milioni 30,6,00,000, ambazo ni mali ya tajiri wake anafahamika  kwa jina la Yussuf Mohamed, ambazo alikuwa anakwenda kuziweka katika Benki hiyo.
Hata hivyo, Kamanda Mkadam, alitoa wito kwa Wananchi wakati wanapokwenda kuweka pesa kuacha kwenda kwa miguu na kuwatumia askari kwani askari wapo kwa ajili yao ili kuimarisha usalama wa raia.

 

Shirika la UNFPA Yakabidhi magari ya Wagonjwa Zanzibar.

Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mh. Rashid Seif  wakati akilijaribu moja ya gari hilo zilizotolewa na UNFPA katika hafla ilizofanyika  Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mh. Rashid Seif wakati akilijaribu moja ya gari hilo zilizotolewa na UNFPA katika hafla ilizofanyika Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.

Na RAMADHANI ALI /MAELEZO ZANZIBAR

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu (UNFPA) limekabidhi  msaada wa magari manne ya Ambulance  kwa Wizara ya Afya ya Zanzibar ambayo yatatumika katika Hospitali nne.

Mwakilishi wa UNFPA Tanzania  Dkt. Natalia Kanem alimkabidhi Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman magari hayo katika sherehe zilizofanyika   Wizarani Mnazimmoja.

Dkt. Natalia alitaka  magari hayo yatumike kwa uangalifu ili  kufikia malengo ya millennia  ya kupunguza idadi ya vifo vya mama wajawazito na watoto wanaozaliwa hasa katika maeneo ya vijijini.

Alisema moja ya sababu inayopelekea vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga ni tatizo la usafiri ambalo linachangiwa na uwezo mdogo wa baadhi ya familia hasa katika maeneo ya vijijini.

Aliongeza kuwa  msaada huo ni  sehemu ya Mpango maalum wa Shirika la Umoja wa  Mataifa  ulioanza  mwaka 2011 na kumalizika Juni 2015  ambao  huenda ukaendelea hadi mwaka 2016 kusadia  masuala ya Afya na Lishe.

Amesema  mpango huo wa miaka minne  ambao unahusisha maeneo  makuu saba unaendeshwa kwa pamoja na Mashirika manne ya Umoja wa Mataifa  ambayo ni WHO, UNFPA, UNICEF na WFPA.

Mwakilishi huyo wa UNFPA amewapongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Jakaya Mrisho Kkwete na Rais wa Zanzibar Dkt Ali Muhamed Sheina kwa juhudi kubwa wanazochukua katika kuimarisha huduma za  mama wajawazito na watoto wachanga.

Aliesema UN inathamini juhudi hizo na  juhudi za kuimarisha uchumi hivyo aliahidi  kuwa wataendelea  kuunga mkono kuhakikisha mama wajawazito na watoto wanaozaliwa wanaendelea kuishi katika mazingira yaliyo  salama.

Waziri wa Afya  Rashid Seif Suleiman, alilishukuru Shirika la UNFPA kwa misaada mbali mbali inayotoa kwa Wizara hiyo  na ameahidi kuwa magari hayo yatatumika katika malengo yaliyokusudiwa.

Amekiri kuwa tatizo la usafiri kwa  mama wajawazito Zanzibar limekuwa likiwasumbua wananchi wengi na inafikia wakati akinamama hujifungua wakiwa kwenye gari  wakati wa kupelekwa Hospitali ambazo hazina stara wala hazifai kwa kazi hiyo.

Alieleza matarajio  yake kuwa tatizo hilo kwa sasa litapungua kwa kiasi kikubwa baada ya kupatiwa msaada huo ambao umekuja wakati muwafaka ambapo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaelekeza juhudi zake kuimarisha  huduma za afya mijini na vijijini.

Gari hazo za ambulance ambazo zitapelekwa katika Hospitali ya Kivunge, Mwembeladu, Mkoani na Micheweni zimegharimu shilingi milioni 245,000,000 za kitanzania.

CHANZO: ZANZINEWS.

Sitta apokea meseji za matusi

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Samuel Sitta.
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Samuel Sitta.

Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta amesema anapokea meseji za simu zaidi ya 50 kwa siku za kumtukana na kusisitiza ataendelea kupambana kuhakikisha Katiba inayopendekezwa inapatikana.

Sitta alitoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma jana wakati akielezea kutoridhishwa kwake na kile alichodai ni namna hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Saed Kubenea inavyopotoshwa na wanaomchukia.

“Kuna baadhi ya vyombo vya habari wananichukia mimi binafsi. Wasichanganye chuki hizo na mchakato wa Bunge Maalumu,” alisema Sitta na kuongeza;

“Mimi napokea matusi kila siku. Meseji zisizopungua 50 viongozi wa Chadema wameweka namba zangu katika tovuti nitukanwe kila siku hilo mimi niko tayari na mnaniona niko safi tu wala sihangaiki nalo.”

“Lakini sasa Bunge Maalumu ni chombo cha kikatiba,  kiko tofauti na mwenyekiti wake. Huwezi kuliadhibu Bunge Maalumu kwa sababu hupendi sura ya mwenyekiti wake,” alisema.

Sitta alienda mbali zaidi na kusema, “Kwa hiyo wale wanaoendeleza hayo mapambano tuendelee na tutaendelea kupambana, lakini kazi ya Bunge Maalumu itaendelea na ndugu zangu Watanzania mjue tunaandaa Katiba safi na rafiki kwa wananchi na itapatikana.”

Sitta alisema baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo ya kesi ya Kubenea dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kumekuwa na tafsiri alizosema ni potofu.

Baada ya maelezo hayo alimpa ruksa AG, Jaji Frederick Werema kutoa ufafanuzi.

Jaji Werema alisema Mahakama Kuu, katika kutafsiri kifungu cha 25(1) (2) inakiri kwamba kuna tofauti kati ya kifungu kilichoandikwa Kiswahili na kile kilichoandikwa Kiingereza.

Alisema Mahakama Kuu katika hukumu hiyo imesema mamlaka ya kuandika Katiba Mpya ina maana ni mamlaka ya kuandika na kupitisha katiba inayopendekezwa kwa ajili ya kupelekwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni.

Mwananchi.

Jaji Warioba: Tutakutana mtaani

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka 19 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dar es Salaam jana.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka 19 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dar es Salaam jana.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba imeondoa mambo manne muhimu yaliyokuwa kiini cha kupata Katiba ya mageuzi.

Akiyataja mambo hayo muhimu ambayo ni maadili ya viongozi wa umma,  madaraka ya wananchi, mgawanyo wa madaraka na muungano. “Tutakutana mtaani. Tume tutaendelea kutetea rasimu yetu na wao wawaeleze wananchi kwa nini wameondoa maoni yao yaliyokuwa katika Rasimu ya Pili ya Katiba,” aliongeza kwa ufafanuzi Jaji Warioba.

Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 19 tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Dar es Salaam jana, Jaji Warioba alisema rasimu hiyo inatofautiana kwa kiasi kikubwa na rasimu iliyotolewa na tume hiyo Desemba mwaka jana.

“Sina hakika kama tutapata Katiba Mpya labda Katiba iliyoboreshwa. Rasimu au Katiba itakayopendekezwa na Bunge Maalumu haitapigiwa kura hadi 2016. Sina hakika kama kura hiyo itapigwa kwa kuwa hakuna maridhiano hasa kuhusu muungano,  rasimu hiyo itaanza kupingwa tangu siku ya kutolewa kwake,” alisema.

Aliongeza, “Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka kesho Katiba Mpya itakuwa agenda, na agenda hiyo inaweza kuigawa nchi. Kuna uwezekano mkubwa kwamba mwaka 2016 badala ya kupiga kura mchakato ukaanza upya.”

Jumatano wiki hii Mwenyekiti wa kamati hiyo, Andrew Chenge aliwasilisha rasimu hiyo bungeni na kueleza kuwa kamati yake imefuta ibara 28 zilizokuwa katika rasimu ya Jaji Warioba na kuacha ibara 47, kuongeza ibara 42 na kurekebisha ibara 186.

Alisema rasimu hiyo ina sura mpya mbili ambazo ni Mamlaka na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na nyingine inayohusu Ardhi, Maliasili na Mazingira ambayo haikuwekwa katika rasimu ya Warioba kwa kuwa si mambo ya muungano.

Rasimu hiyo ilirejesha muundo wa Serikali mbili kama ilivyo sasa na kutupilia mbali muundo wa Serikali tatu uliopendekezwa na Tume ya Jaji Warioba.

Huku akiwa makini, Jaji Warioba ambaye alitumia saa 1:02 kufafanua umuhimu wa mambo manne yaliyoachwa katika rasimu iliyotolewa na Bunge la Katiba, alisema hivi sasa wajumbe wa Bunge la Katiba wana msemo wao kuwa “Warioba ni shida”, kufafanua kuwa watakapomaliza vikao vya Bunge hilo Oktoba 4, mwaka huu na kurejea mtaani walipo wananchi ndiyo watajua nani ni ‘shida’, kati yake na wao.

Akizungumzia kitendo cha Bunge hilo kubadili kanuni ili kuruhusu wajumbe wake kupiga kura za kupitisha rasimu hiyo kwa baruapepe (e-mail) na nukushi (fax) wakiwa nje ya nchi, Jaji Warioba alisema, “Utaratibu huu hauwezi kutuletea Katiba ya maridhiano. Hata mimi nimeanza kukata tamaa.”

Huku akishangiliwa kila mara na mamia ya watu waliohudhuria kongamano hilo, wakiwamo wasomi na baadhi ya waliokuwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba alisema kila mjumbe wa tume hiyo alikuwa na mawazo yake juu ya Katiba, lakini waliweka kando mawazo yao baada ya kusikia kauli za Watanzania juu ya Katiba wanayoitaka.

Katika maadhimisho hayo,  Jaji Warioba pia alizindua kitabu cha marehemu Dk Sengondo Mvungi kiitwacho ‘Mvungi anapumua Katiba’. Dk Mvungi  aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Katiba na mmoja wa waanzilishi wa LHRC, alifariki dunia mwaka jana nchini Afrika Kusini alikopelekwa kutibiwa baada ya kujeruhiwa na majambazi akiwa nyumbani kwake.

Maadili ya Viongozi wa umma

Kuhusu maadili ya viongozi wa umma alisema, “Wananchi walitoa maoni mazito kuhusu maadili ndani ya jamii na maadili ya viongozi. Kutokana na maoni ya wananchi Tume iliimarisha misingi mikuu ya taifa iliyo katika Utangulizi wa Rasimu. Misingi iliyo katika katiba ya sasa ni uhuru, haki, udugu na amani.”

Alisema kutokana na maoni ya wananchi misingi mipya iliongezwa ambayo ni;  utu, usawa, umoja na mshikamano na kwamba wananchi pia walipendekeza tunu za taifa ziwekwe kwenye katiba ambazo ni utu, uzalendo, uadilifu, umoja, uwazi, uwajibikaji na lugha ya Taifa (Kiswahili ).

“Bunge Maalumu limeondoa uadilifu, uzalendo, umoja, uwazi, na uwajibikaji kutoka kwenye orodha ya tunu za taifa na kuziweka kwenye misingi ya utawala bora. Kila Mtanzania anatakiwa awe mzalendo, kila Mtanzania anatakiwa kuwa mwadilifu, kila Mtanzania anatakiwa aenzi umoja. Inakuwaje mambo haya yahusu utawala tu?” alihoji.

Alisema tunu za taifa ndiyo msingi wa utamaduni na maadili ya taifa, kwamba mwelekeo wa taifa utategemea jinsi wananchi wanavyoenzi misingi mikuu na tunu.

Aliponda kitendo cha Bunge la Katiba kutoweka miiko ya uongozi kwenye Katiba wakati kila siku viongozi wanalalamika juu ya rushwa na ufisadi, pamoja na fedha za umma kuwekwa kwenye akaunti za benki nje ya nchi.

“Katika bara la Afrika, nchi kama Afrika Kusini, Namibia na Kenya zimeweka misingi ya maadili na miiko katika Katiba. Hapa kwetu sheria tulizonazo haziwezi kupambana na rushwa na ufisadi. Sijui kwa nini Bunge la Katiba wameondoa hili,” alisema.

Madaraka ya Wananchi

Jaji Warioba alipinga kitendo cha Bunge la Katiba kuondoa kipengele cha wananchi kuwa na madaraka ya kumwondoa mbunge wao kama hawaridhishwi na uwakilishi wake bungeni, mbunge kutokuwa waziri ili aweze kuwawakilisha vizuri na ukomo wa mbunge kuwa vipindi vitatu .

“Bunge lina kanuni za kuwawajibisha wabunge na wananchi nao wanapenda kuwa na madaraka hayo. Vyama vya siasa vina madaraka ya kuwaondoa wabunge wao katikati ya kipindi. Wananchi nao wanataka watumie madaraka yao,” alisema.

Mgawanyo wa madaraka

Akizungumzia mgawanyo wa madaraka kati ya mihimili ya Bunge, Serikali na Mahakama, alisema pendekezo lao la kumwondoa rais na mawaziri kutoka kwenye Bunge linakataliwa kwa sababu nchi imezoea mfumo wa kibunge kama ilivyo kwa nchi nyingi za jumuiya ya madola.

“Siyo kweli kwamba mfumo wetu ni wa kibunge. Kwenye mfumo wa kibunge mkuu wa nchi hana madaraka ya utendaji. Madaraka hayo yako mikononi mwa Waziri Mkuu ambaye ni mbunge. Hivyo ndivyo ilivyo kwa Uingereza, India, Canada, Australia, New Zealand,” alisema.

Akitolea mfano mwingiliano huo alisema wakati wa kutunga Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, bunge lilitunga sheria lakini baadaye Rais alifanya mazungumzo na watu nje ya bunge na baadaye bunge likalazimika kubadili uamuzi.

 “Tanzania ina mfumo wa urais ambapo rais ni mkuu wa nchi, mtendaji mkuu na amiri jeshi mkuu. Rais na mawaziri wake kuwa sehemu ya bunge ni kuchanganya mamlaka. Hali hii inafanya Serikali kuingilia mamlaka ya bunge na pia bunge kuingilia mamlaka ya Serikali,” alisema.

Aliongeza, “Nchi nyingi zimebadili Katiba zao ili kutenganisha madaraka ya mihimili. Jirani zetu wa Msumbiji na Kenya wamefanya hivyo. Kenya imefanya hivyo na sababu zao zinafanana kabisa na zile ambazo wananchi wa Tanzania walitoa.”

Muungano

Huku akitaja kero 20 za muungano, 11 za Zanzibar na 10 za Tanzania Bara zilizotajwa na wananchi wakati wa kukusanya maoni, Jaji Warioba alisema, “Ingawa Rasimu ya Bunge Maalumu limerudisha madaraka ya rais kuigawa nchi hiyo peke yake haitoshi. Mambo haya ni magumu kubadilika kwa upande wa Zanzibar.”

Aliongeza kuwa ili kufanya mabadiliko kwenye Katiba ya Zanzibar ni lazima mabadiliko yapitishwe kwa theluthi mbili au zaidi ya Wawakilishi.

Mwananchi.